Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa BAKWATA yatikiswa bungeni
Habari za SiasaTangulizi

BAKWATA yatikiswa bungeni

Baadhi ya wabunge wa Upinzani katika Bunge lililopita
Spread the love

MBUNGE wa Ubungo (CHADEMA), Saed Kubenea, amehoji hatua ya serikali ya kulipa mamlaka ya mwisho ya kupeleka mahujaji nchini Saudia, Baraza Kuu la Waislamu (BAKWATA). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza bungeni mara baada ya kumalizika kipindi cha maswali na majibu leo Jumatatu, tarehe 7 Mei, Kubenea amesema, “serikali imetoa mamlaka ya mwisho ya kupeleka mahujaji nchini Saudia Bakwata ili kutimiza nguzo kuu ya uislamu.”

Amesema, “jambo hili ni kinyume na Ibara ya 63 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Hatua hii, ni kinyume na sheria za nchi na kinyume na matakwa ya uislamu na waislamu.

“Hivyo basi, kwa kuwa Bunge ndio chombo kikuu cha wananchi kwa mujibu wa Katiba; chombo hiki kwa mujibu wa Katiba, ndicho kinachosimamia serikali na kuishauri kwa niaba ya wananchi, naomba serikali itueleze kwa nini imetoa mamlaka haya kwa BAKWATA, wakati chombo hiki siyo mali ya waislamu wote?”

Akizungumza kwa hisia kali, Kubenea alisema, “Katiba ya Jamhuri ya Muungano, inatamka kuwa serikali haina dini. Lakini serikali hii, imejiingiza kwenye mambo ya dini na kutaka waislamu wote kwenda Hijja kupitia Bakwata.”

Amesema, “taifa hili lina taasisi 11 zenye usajili sawa kama Bakwata. Kuwalazimisha waislamu wote kutumia Bakwata kwenye mambo ya Hijja, ni kinyume na katiba. Haikubariki.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!