Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Babu Seya atinga Ikulu kumshukuru Rais Magufuli
Habari za Siasa

Babu Seya atinga Ikulu kumshukuru Rais Magufuli

Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza wakiwasili Ikulu
Spread the love

Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha” Francis Nguza na Michael Nguza leo wamefika Ikulu kumshukuru Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa msamaha aliotoa kwao dhidi ya kifungo cha maisha walichokuwa wakitumikia gerezani, anaandika Hamis Mguta.

Rais Magufuli alitoa msamaha huo Disemba 9 mwaka jana, akiwa Dodoma katika sherehe za miaka 56 ya Uhuru.

Mwaka 2003, Babu Seya na wanaye watatu walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kubaka na kulawiti watoto wa Shule ya Msingi Mashujaa ambapo mwaka 2004, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar iliwahukumu wote wanne kifungo cha maisha jela.

Baada ya hukumu hiyo, walikata rufaa lakini mwaka 2005, Mahakama Kuu iliridhia hukumu hiyo ya kifungo cha maisha jela kwa wote wanne kabla ya Mahakama ya Rufaa kuwaachia huru watoto wawili wa Nguza – Mbangu “Nguza Mashine” na Francis  Nguza “Chichi” mnamo Februari 2010.

Nguza amesema “Muheshimiwa rais alinisamehe kule, nimekuja kutoa shukrani zangu za dhati kutoka ndani ya moyo wangu na kumuomba aniruhusu sasa kuanza kufanya kazi.

“Kuanzia sasa nipo huru kufanya kazi, mashabiki wanipe muda kidogo nitawatangazia lini nitanza kuingia jukwaani.”

 

1 Comment

  • Rais amewasamehe kama alivyodai kwa mujibu wa sheria. Asimsingizie Mungu kuwa ndiye aliyesamehe
    Lakini kina Babu Seya nao wameomba msamaha kwa watoto waliowalawiti? Utamsamehe vipi mtu ambaye hajaomba msamaha?
    Nashauri Rais sasa akutane na watoto waliolawitiwa na wazazi wao. Hawa ndio waliodhulumiwa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!