Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Baada ya Zahera, Yanga wavunja Kamati ya Mashindano
Michezo

Baada ya Zahera, Yanga wavunja Kamati ya Mashindano

Hassan Bumbuli, Afisa Habari wa Yanga
Spread the love

KAMATI ya Utendaji ya Klabu ya Yanga, imeivunja Kamati ya Mashindano ya klabu hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 7 Novemba 2019, na Hassan Bumbuli, Afisa Habari wa Klabu ya Yanga, kamati hiyo ilivunjwa rasmi tarehe 2 Novemba,  mwaka huu.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, uamuzi wa kamati hiyo kuvunjuwa, ulifikiwa kwenye kikao cha Kamati ya Utendaji  kilichoketi katika makao makuu ya klabu ya Yanga Jangwani, jijini Dar es Salaam, chini ya Dk. Mshindo Msolla, Mwenyekiti wa klabu hiyo.

“Uamuzi wa kuivunja kamati ya mashindano, ulifikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji kilichoketi Novemba 2, 2019 makao makuu ya klabu, “ inaeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imesema kamati mpya ya mashindano itatangazwa baadae na uongozi wa klabu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!