BAADA Ya kuifunga klabu ya Simba na kuchukua ubingwa wa kombe la Mapinduzi kwa mara ya tatu, rekodi pekee iliyowekwa na klabu ya Azam Fc katika michuano hiyo ya mwaka huu ni kucheza jumla ya michezo mitano bila kufungwa wala kuruhusu goli lolote, anaandika Kelvin Mwaipungu.
Goli pekee la Azam Fc katika fainali iliyopigwa jana lilifungwa na kiungo mkabaji Himid Mao kwa shiti la umbali wa mita 25, na kuipa klabu hiyo taji la tatu la michuano hiyo ya Mapinduzi inayofanyika kila mwaka visiwani Zanzibar.
Katika michuano hiyo Azam Fc ilicheza michezo yote bila kuruhusu goli hata moja, mchezo wa kwanza Azam Fc, ilicheza na timu ya Zima moto na kuibuka na ushindi wa bao moja kwa bila na kwenda sare katika mchezo wa pili dhidi ya Jamhuri na baadae kuipa kipigo kikari Yanga cha mabao 4-0 na kufanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali na kupata ushindi wa bao moja mbele ya Taifa Jang’ombe na baadae kucheza fainali dhidi ya Simba.
Azam Fc ambayo katika michuano hiyo iliongozwa na kocha wake wa muda Iddi Cheche ambaye alikuwa akifundisha timu ya vijana, baada ya kutimua jopo la makocha kutoka nchini Hispania kutokana na mwenendo mbaya wa timu katika michezo ya ligi kuu.
Leave a comment