Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Auawa kwa tuhuma za ujambazi
Habari Mchanganyiko

Auawa kwa tuhuma za ujambazi

Spread the love

MTU mmoja anayefahamika kwa jina la Mussa Faustine (19) mkazi wa Bugarika wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza, ameuawa na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za ujambazi. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 28 Julai, 2018, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi amesema Faustine amefariki dunia akiwa njiani kuelekea hospitali kutokana na majeraha ya kipigo cha wananchi,  baada ya kuhojiwa na askari polisi.

Kamanda Msangi amesema kabla ya mtuhumiwa huyo umauti kumfika aliutaja mtandao sugu wa ujambazi na kiongozi wake anayefahamika kwa jina la Hamza, ambao ulipanga kutekeleza matukio mengine ya ujambazi hivi karibuni.

“Kijana huyo alitoa ushirikiano vizuri kwa askari japo alikuwa katika hali ya kujeruhiwa sana, alitoa ushirikiano na kueleza kikundi chake ambacho wanashirikiana katika kufanya na kupanga matukio ambayo walikuwa wamepanga kufanya katika siku za hivi karibuni kisha alimtaja kiongozi wake aitwaye hamza maarufu mjomba,” amesema Kamanda Msangi.

Vile vile, Kamanda Msangi amesema marehemu Faustine aliwapeleka polisi maeneo wanakoficha silaha, ambapo polisi baada ya kufanya upekuzi walikuta silaha nne zilizotengenezwa kienyeji na risasi saba.

Kamanda Msangi amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa ajili ya uchunguzi na kwamba uchunguzi ukikamilika utakabidhiwa kwa ndugu zake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!