Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Gwajima amfananisha Rais Magufuli na Nabii
Habari za Siasa

Askofu Gwajima amfananisha Rais Magufuli na Nabii

Spread the love

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Dk. Josephat Gwajima amemfananisha Rais John Magufuli na Nabii. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akichangia hoja katika mkutano wa wadau wa sekta ya madini uliofanyika leo tarehe 22 Januari 2019 jijini Dar es Salaam, Askofu Gwajima amesema Rais Magufuli amekuwa kama nabii.

“Ahsante sana rais leo umekuwa kama nabii, wakati nimekaa hapa nilisema itawezekanaje nitoke hapa bila kuongea, ingekuwa shida,” amesema Gwajima.

Akichangia kuhusu changamoto zianzoikabili sekta ya madini hapa nchini, Askofu Gwajima ameishauri serikali kuunda timu ya watu wenye uwezo na ushawishi wa kumudu siasa za kibiashara katika kiwango cha kimataifa hasa kwenye kutafuta masoko ya madini nje ya nchi.

“Si kweli hakuna soko la madini, sababu dhahabu yenyewe ni fedha ukiwa nayo ni fedha, isipokuwa tu nilikuwa nashauri, uwe na watu wenye exposure na siasa ya madini, kuunda watu wenye akili na wenye exposure ambao wanaweza kuziikia nchi mbalimbali dunia kutafuta masoko

Kuhusu changamoto ya uwepo wa kodi katika biashara ya madini, Gwajima amesema hashauri kupunguzwa kwa kodi bali serikali iwapunguzie kiwango cha kodi kwa wachimbaji wenye kiwango kidogo cha madini.

“Nilipita Mwadui njiani Maganzo nilishangaa kweli, nikapaki gari watu wakasema huyu Gwajima wakanifuata wakitaka kuniuzia dhahabu, ndani ya saa moja nililetewa bakula la ilog tano limejaa Almasi. Hizi kama zingelipiwa ushuru nchi yetu ingefika mbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!