Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Anglikana: Kwaresma iwe ya toba
Habari Mchanganyiko

Askofu Anglikana: Kwaresma iwe ya toba

Spread the love

ASKOFU wa Kanisa la Anglikana, Jimbo la Central Tanganyinya Dk. Dickson Chilongani, amewataka waumini wa Kikristo kutumia vyema kipindi cha Kwaresma kwa kuwasaidia wahitaji. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Amesema, kipindi cha Kwaresma kiwe kipindi cha toba ambacho kinaambatana na kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani yatima, wajane na watu wanaoishi katika mazingira magumu.

Ametoa kauli hiyo tarehe 26 Februari 2020, wakati wa ibada ya kupaka majivu, muda mfupi baada ya kumalizika kwa mahubiri yaliyofanyika katika Kanisa la Anglikana linalojulikana kama Kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Jijini Dodoma.

Amesema, kipindi hiki cha kukumbika mateso ya Yesu Kristo, kiwe kipindi cha kufanya maombi ya toba kwa mtu mmoja mmoja, familia, jamii inayomzunguka pamoja na kuliombea taifa.

Naye Mchungaji Canon Jonas Mdumulla ambaye ni kiongozi wa ibada wa kiingereza akihubiri kanisani hapo, amewataka waumini wote wa Kikristo kujiepusha na maovu na badala yake wawe watu wa kuomba toba.

Pamoja na kuwataka kujiepusha na uovu na kuomba toba, pia amewakemea baadhi ya Wakristo wanaoacha dhambi katika kipindi cha Kwaresma pekee na kisha wanarudia kutenda.

“Kwa sasa kuna watu ambao wamejinyenyekeza, lakini kipindi hiki cha majivu kikiisha, wanarudia kutenda dhambi wengine wanachukua au kutoa rushwa.

“Unapokuwa kwa Kristo, unatakiwa kuwa moja kwa moja hakuna kupwa na kujaa pamoja na kuwa yapo mapito mbalimbali pamoja na majaribu lakini njia pekee ni kufanya maombi ambayo yatakuvusha katika mapito yako,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!