Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko ASAS wagawa maziwa kwa Wabunge kuhamasisha unywaji
Habari Mchanganyiko

ASAS wagawa maziwa kwa Wabunge kuhamasisha unywaji

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (kulia) akipokea maziwa aina ya Asas Dairies Milk kutoka kwa Mshauri wa Kampuni hiyo, Abdul Ally
Spread the love

WATANZANIA wamehamasishwa kutumia maziwa kwa wingi ili kuweza kutunza afya zao kutokana na kuwa maziwa hayo yanapaikana. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Wito huo umetolewa na Mshauri wa Kampuni ya Asas Dairies Milk, Abdul Ally wakati akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega pamoja na baadhi ya wabunge akiwemo mbunge wa Viti Maalum, Mariam Ditopile (CCM). 

Akizungumza kuhusu matumizi ya maziwa alisema kuwa kampuni hiyo imekuwa ikizalisha maziwa ambayo kimsingi yameboreshwa sambamba na kusambaa katika nchi nzima.

Amesema kuwa kwa sasa kampuni hiyo imekuwa ikifanya kampeni ya kusambaza maziwa hayo katika taasisi mbalimbali ikiwa pamoja na kusambaza katika shule za msingi na sekondari.

Naye mwakilishi wa Kampuni hiyo mkoa wa Dodoma, Lupyana Chagula, alisema kampuni hiyo imeona ni vema kupeleka maziwa bungeni ili kuhamasisha unywaji wa maziwa sambamba na kuchochea matumizi ya mazao ya maziwa ambayo ni bidhaa za ndani badala ya kusubiri bidhaa hiyo kutoka nje.

Kwa upande wake, Waziri Ulega alisema kampuni hiyo imekuwa ikijitahidi kuhamasisha unywaji wa maziwa na yamekuwa yakipendwa na wanywaji na kusababisha kuongeza hamasa ya unywaji wa maziwa kwa jamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!