Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Michezo Arsenal waipiga Chelsea, watwaa ubingwa FA CUP
Michezo

Arsenal waipiga Chelsea, watwaa ubingwa FA CUP

Spread the love

PIERRE- Emerick Aubameyang, kiungo mshambuliaji wa Arsenal ameiwezesha timu yake kutwaa ubingwa wa Kombe la FA CUP nchini Uingereza kwa kuofungia magoli 2-1 dhidi ya Chelsea. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea)

Aubameyang amefunga magoli hayo moja kwa penati dakali ya 28 baada ya kuchezewa rafu ndani ya 18 na beki wa Chelsea Cesar Azpilicueta na kuzawadiwa kadi ya njano.

Goli hilo lilikuwa la kusawazisha baada ya Chelsea kuongoza Christian Pulisic kufunga dakika ya 5 ya mchezo huo uliopigwa dimba la Wembley.

Dakika ya 68, Aubameyang raia wa Gabon aliifungia Arsenal goli la pili akipokea pasi safi kutoka kwa Nicholas Pepe.

Chelsea iliwalazimu kucheza wakiwa pungufu kuanzia dakika ya 72 baada ya kiungo wake, Mateo Kovacic kuzawadia kadi ya pili ya njano kwa kumchezea rafu kiungo wa Arsenal, Granint Xhaka.

Arsenal wametwaa taji hilo kwa mara ya 14 ambapo mara ya mwisho ililitwaa taji hilo mwaka 2017.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Tusua kijanja na mechi za Europa leo

Spread the love  Alhamisi ya leo EUROPA inaendelea ambapo ni mechi za...

Michezo

Hapa Diego Simeone, pale Simeone Inzaghi kivumbi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya

Spread the love LIGI ya Mabingwa ulaya itaendelea usiku wa leo ambapoitakwenda...

error: Content is protected !!