Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Ander Herrera kutembelea Tanzania
Michezo

Ander Herrera kutembelea Tanzania

Ander Herrera
Spread the love

KIUNGO wa Manchester United na  Hispania, Ander Herrera anatarajiwa kutembelea nchi mbili zilizopo kwenye Ukanda wa Afrika ya Mashariki ikiwemo Tanzania bila kuweka wazi sababu zitakazomfanya kuja  wala kutaja muda gani atakaotua nchini.

Herrera ameandika haya kwenye ukurasa wake mtandao wake wa Twitter baada ya kuulizwa swali na moja ya mashabiki zake, Je ni sehemu gani ya dunia unayopenda kutembea na lakini haujawahi kuwa awali?

Kiungo huyo alitaja nchi nne ambazo ana mpango wa kuzitembelea kwa siku za hivi karibuni lakini katika Ukanda wa Afrika Mashariki anatamani kutembelea Kenya na Tanzania, na nyingine zikitokea America ambazo ni Colombia na Argentina.

https://twitter.com/AnderHerrera/status/817456499417055232

Tamaa ya mchezaji huyo kuja nchini, huwenda ikawa imechagizwa na ziara iliyofanywa na magwiji wa klabu ya FC Barcelona waliokuja nchini Machi 28, 2015 na kutembelea vivutio vya ndani baada ya kucheza mchezo katika uwanja wa Taifa dhidi ya Maveterani wa Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!