Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Anayedaiwa kutumia jina la Katibu Mkuu CCM kutapeli akamatwa
Habari Mchanganyiko

Anayedaiwa kutumia jina la Katibu Mkuu CCM kutapeli akamatwa

Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Wilfred Welandumi kwa madai ya kutumia jina la Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kufanya utapeli. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo tarehe 5 Aprili 2019, SACP Lazoro Mambosasa, Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema, jeshi hilo limemwanika Welandumi (40) ili kuwapa wananchi tahadhari.

Kamanda Mambosasa amesema, Welandumi ni mkazi wa Yombo, Dar es Salaam.

“Mtuhumiwa huyo amekuwa akiwapigia simu baadhi ya wabunge wa chama tawala na kuwaomba fedha kwa kujifanya yeye ni Dk. Bashiru na hatimaye kufanikiwa kutapeli fedha kiasi cha Tsh. 370,000,” amesema.

Na kwamba, mtuhumiwa huyo hakutumia jina la Dk Bashiru pekee yake bali hata jina Prof. Makame Mbarawa ambaye sasa ni Waziri wa Maji.

Mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!