Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Amnesty: Kunyamazisha wakosoaji ni tusi
Habari za Siasa

Amnesty: Kunyamazisha wakosoaji ni tusi

Spread the love

KUENDELEA kuwekwa kuzuizini kwa mwanasheria wa haki za binadamu, Tito Elia Magoti na mwenzake Theodory Giyani, ni jaribio la kutaka kunyamazisha wakosoaji. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ni kauli ya shirika la lisilo la kiserikali la masuala ya haki za binadamu la kimataifa – Amnesty International, tarehe 21 Januari 2020, wakati watuhumiwa walipofikishwa mahakamani.

Tito na Giyani, ambao ni wayefanyakazi kwenye Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), walifikishwa katika Mahakama ya Kisutu kwa tuhuma za kuongoza genge la uhalifu, kumiliki programu ya kompyuta iliyobuniwa kwa lengo la kutenda uhalifu na utakatishaji fedha.

“Ni tusi kwa haki na ni jaribio la wazi la kuwanyamazisha wakosoaji wa serikali kwa kuwaweka kizuizini,” taarifa ya shirika hilo imeeleza, kwa mara ya kwanza walishikiliwa tarehe 20 Desemba 2019.

Amnesty imeeleza kuchukizwa na matumizi ya sheria ya kushughulikia uhalifu, kwa kuwaweka ndani wakosoaji kwa muda mrefu kwa makosa yasiyo na dhamana, kwa madai ya kutokamilika upelelezi.

“Kufanya hivi ni kukiuka kabisa utaratibu unaozingatia sheria na upotoshaji wa haki,” amesema Seif Magango, Naibu Mkurugenzi wa Amnesty International katika Kanda ya Afrika Mashariki kwenye taarifa hiyo na kuongeza kuwa mamlaka husika zinapaswa kuwaacha Magoti na Giyani bila masharti.

Tito na Giyani walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tarehe 24 Desemba 2019, na kusomewa mashtaka matatu ambapo tarehe 7 Januari 2020, mahakama ya jijini Dar es Salaam iliahirisha kesi yao baada ya upande wa mashtaka kuomba muda zaidi wa kukamilisha upelelezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!