Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Al-Shabab yatia doa uchaguzi Kenya
Makala & Uchambuzi

Al-Shabab yatia doa uchaguzi Kenya

Askari wa Al-Shabab
Spread the love

ZIKIWA zimebaki siku tano kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu nchini Kenya, hali ya usalama imeendelea kuwapa wasiwasi wananchi kufuatia mashambulizi pembezoni mwa pwani ya nchi hiyo, anaandika Catherine Kayombo.

Mashambulizi hayo yamefanyika maeneo ya Lamu, Mandera na maeneo ya jimbo la Lafey na wa watu wanaohisiwa kuwa Al-Shabab. Watu hao wamefanya mashambulizi ya mfululizo kwa siku mbili jumatano na Alhamis wakisababisha vifo vya watu takriban wanane.

Washambuliaji hao walivamia basi la abiria jana katika eneo la Lamu na kujeruhi watu watano. Pia Alhamis walivamia offisi za polisi katika Jimbo la Lafey na kuua polisi huku wengine wakijeruhiwa.

Kufuatia mashambulizi hayo, wakazi wa Pwani wamepata wasiwasi juu ya usalama wao kuelekea uchaguzi, kupelekea wengine kukimbia makazi yao. Wametoa rai kwa serikali kutozembea katika ulinzi hasa katika maeneo yanayoonekana kuwa hatarishi na yenye historia ya kuvamiwa na waasi.

Aidha, katibu katika wizara ya usalama joseph Bonieth amewahahakikishia wakazi wa Lamu na Mandera kuwa serikali itahakikisha ulinzi unakuwepo, na watu wasihame wala kukimbia maeneo yao kuhofia uvamizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Miaka 28 watumishi UDSM yaliwa na nzige, madumadu

Spread the loveGEORGE Francis anasikitika; anatembea akiwa na mawazo mengi, hajui la...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nimekumbuka Samia wa miaka 3 iliyopita

Spread the loveWAKATI naandaa makala ya safu hii wiki hii, nimejikuta nakumbuka...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Hakuna fedha za Rais

Spread the loveKUNA mambo machache mazuri ya kujifunza kutoka kwa Margaret Thatcher,...

error: Content is protected !!