Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ajali ya Ndege Serengeti: Wawili wafariki
Habari Mchanganyiko

Ajali ya Ndege Serengeti: Wawili wafariki

Ajali ya Ndege
Spread the love

WATU wawili wamefariki dunia katika ajali ya ndege iliyotokea asubuhi ya leo tarehe 23 Septemba 2019, kwenye uwanja wa ndege mdogo wa Seronera uliko kwenye hifadhi ya Serengeti mkoani Mara. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa ya ajali hiyo imetolewa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Taarifa ya TANAPA inaeleza kuwa, ajali hiyo imetokea baada ya ndege ndogo ya Kampuni ya Auric Air kuanguka katika uwanja wa Seronera.

“Ndege ya Kampuni ya Auric Air imeanguka leo asubuhi katika uwanja mdogo wa ndege Seronera, Serengeti. Rubani mmoja na abiria mmoja wamepoteza maisha. Taarifa zaidi zitatolewa.Rubani na abiria wote ni raia wa Tanzania,” inaeleza taarifa ya TANAPA.

Pascal Shelutete, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Mawasiliano TANAPA amesema ndege hiyo ilikuwa na watu wawili ambao wote wamefariki dunia.

Shelutete amesema, mamlaka husika zitatoa taarifa zaidi juu ya chanzo cha ajali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!