Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ajali mbaya yatokea Songwe, yaua abiria wote
Habari Mchanganyiko

Ajali mbaya yatokea Songwe, yaua abiria wote

Spread the love

WATU 19 wamepoteza maisha kutokana na ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika eneo la Senjele mkoani Songwe. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akithibitisha kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Songwe, SACP, George Simba Kiando amesema ajali hiyo iliyohusisha lori lenye namba za usajili T825 CMJ na gari la abiria aina ya Coaster (T269 CJC), ilitokea majira ya saa tatu na robo usiku.

Kamanda Kiando amesema chanzo cha ajali hiyo ni breki ya Lori kushindwa kufanya kazi katika mteremko wa mpakani mwa mkoa wa Mbeya na Songwe na kulikopelekea roli hilo kuigonga Coaster iliyokuwa na abiria 18 na kusababisha vifo hivyo.

Ameeleza kuwa, watu 17 akiwemo dereva wa roli walifariki papo hapo wakati wawili walifariki dunia wakati wakipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Kamanda Kiando amesema katika vifo hivyo, watu 14 walikuwa wanawake na 5 walikuwa wanaume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!