Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Afya ya Bulaya yaimarika Muhimbili
Habari za Siasa

Afya ya Bulaya yaimarika Muhimbili

Spread the love

ESTHER Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anaendelea na matibabu katika hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kufikishwa hospitalini hapo jana, anaandika Irene Emmanuel.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, John Stephen, Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili amesema, Bulaya anaendelea na matibabu na hali yake ni nzuri.

“Esther Bulaya aliletwa hapa kwetu jana usiku saa tano, na alitokea hospitali ya wilaya ya Tarime, yuko hapa na anaendelea vizuri na matibabu lakini hatuwezi kuweka wazi nini kinamsumbua, ” alisema

Bulaya alikimbizwa hospitalini jana baada ya kuzidiwa na kupoteza fahamu akiwa rumande alikokuwa ameshikiliwa na jeshi la polisi Kanda Maalum ya Tarime akituhumiwa kuhutubia mkutano wa hadhara nje ya jimbo lake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!