MAHAKAMA Kuu kanda ya Dar es Salaam imekiruhusu chama cha ACT-Wazalendo kulishtaki Jeshi la Polisi Tanzania kwa kuzuia ziara za chama hicho. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Kesi hiyo namba 8 ya mwaka 2018 imepangwa kuanza kusikilizwa Aprili 4, mwaka huu mbele ya Jaji Ferdinand Wambari, Jaji Rehema Sameji, na Jaji Rose Teemba.
Chama hicho kimefunga shauri hilo kwa lengo la kulishtaki jeshi hilo kuacha kuingilia shughuli za chama hicho isivyo halali.
Frebruari 23 mwaka huu Kiongozi wa chama hicho Zitto Kabwe alitiwa mbaroni na jeshi la Polisi mkoani Morogoro kwa kudaiwa kufanya ziara kinyume na sheria.
Leave a comment