Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Membe ni mtaji kwetu
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo: Membe ni mtaji kwetu

Spread the love

BERNARD Membe, aliyekuwa mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na Waziri wa Mambo ya Nje Nje katika Serikali ya Awamu ya Nne, ni mtaji katika chama chetu. Anaripoti Hamis Mguta, Mafia…(endelea).

Hiyo ni kauli ya Nasir Abubakari, Katibu wa Uenenzi wa Chama cha ACT-Wazalendo wilayani Mafia alipozungumza na mwandishi wa MwanaHALISI Online.

“Membe ni mtu ambaye anaonekana kuwa na busara kubwa kwasababu tangu afukuzwe kwenye chama chake, ametumia muda mrefu kutafakari na wala hajakurupuka,” amesema.

Abubakari ambaye ni metia nia ya kugombea udiwani wa Kata ya Kiegeani, Mafia kupitia chama hicho katika uchaguzi wa Oktoba 2020, ameuambia mtandao huu kwamba wanamkaribisha Membe kwa mikono miwili.

“Nimesikia amerudisha kadi na kama atakuja ACT-Wazalendo, basi nami naungana na wakuu wangu wa chama Maalim Seif na Zitto Kabwe kwamba aje, akufanya hivyo atakuwa amefanya maamuzi ya busara na hekima.

“Naamini Membe ana mtaji wa watu, atakuja na mtaji ambao ametoka nao CCM, wao wamemfukuza uanachama lakini ni kumzalilisha tu, mtu ambaye ameshika nafasi mbakimbali katika serikali na amefanya mambo makubwa, kitendo cha kumfukuza sio cha kiungwana, tunamkaribisha aje tuitengeneze Tanzania yetu,” anasema Abubakari.

Hata hivyo, Abubakari amesisitiza kuwa, kitendo cha vyama vya upinzani kuungana katika uchaguzi wa mwaka huu ni jambo litakalounganisha nguvu, pia itasaidia kama ilivyokuwa mwaka 2015 wakati alipokuwa kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Anasema katika uchaguzi wa mwaka 2020 Membe akipewa nafasi ya kupeperusha bendera ya urais kwa umoja wa vyama vya upinzani kama ilivyokuwa kwa Lowassa mwaka 2015, upinzani utachukua nchi kama Malawi.

“Membe akija ni kuchukua serikali tu, kwasababu wananchi wanamuhitaji, Malawi yamefanyika upinzani unaongoza nchi kwanini sisi tushindwe? Tusitishwe ya kwamba kutakuwa na vurugu, hapana”. anasema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!