KWA mara nyingine mnada wa kuuza nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi umeshindwa kufanikiwa baada ya wateja wengi kutofikia bei inayotakiwa, anaandika Mwandishi Wetu.
Katika mnada uliopita nyumba hizo hazikununuliwa baada ya mmoja wa wateja waliozitaka, Dk. Luis Shika kwa jina marufu ‘900 inapendeza’ kupandisha bei hadi Sh. 900 milioni, lakini alipotakiwa kulipa asimilia 25 kama sehemu ya malipo alishindwa kwa madai kwamba fedha zake nje ya nchi.
Hata hivyo, leo mnada huo umerudiwa tena na nyumba iliyopo kitalu 47 Mbweni JKT imeshindwa kununuliwa kutokana na wateja kuhsindwa kufikia bei elekezi.
Leave a comment