Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Naibu Waziri aimwagia sifa CCBRT
Afya

Naibu Waziri aimwagia sifa CCBRT

Spread the love

NAIBU Waziri wa Afya Dk. Godwin Mollel ameipongeza hospitali ya CCBRT kwa utendaji kazi mzuri licha ya kuwepo changamoto zinawaikabili hospitali hiyo. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam …. (endelea).

Waziri Mollel ameyasema hayo alipotembelea hospitali hiyo leo tarehe 1 Julai 2020 iliyoko Msasani jijini Dar es Salaam katika ziara isiyo rasmi na kukutana na kusalimiana na uongozi wa hospitali hiyo.

Amesema kuwa ameamua kuitembelea hospitali hiyo kwakuwa imekuwa ikiendelea kushirikiana na Serikali kwa muda mrefu kutoa huduma bora za  afya kwa watanzania wenye mahitaji. 

“Nawafahamu CCBRT na kazi mnazozifanya kwa muda mrefu sasa, nawapongeza kwa kazi nzuri, kama Serikali tunatambua mchango wa hospitali hii katika kuwahudumia watanzania, leo nimefika kusalimia kidogo lakini naahidi kuja rasmi ndani ya kipindi cha mwezi mmoja ili tuweze kupata wasaa wa kujadilina kwa kina juu ya kazi zenu,” amesema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Hospitali hiyo, Brenda Msangi amemshukuru Dk. Mollel kwa kufika CCBRT, na kumueleza ambavyo taasisi yake inanufaika na ubia kati yake na serikali tangu kuanza kwake hadi hapa ilipofikia.

“Kwa niaba ya wafanyakazi wenzangu wa CCBRT napenda kuchukua nafasi hii kuishukuru Serikali yetu kupitia Wizara ya afya tumekuwa tukipata msaada na ushirikiano mkubwa  kutoka serikalini kwa hili, nasema asante sana na naomba utufikishie salam zetu kwa dada yangu Ummy Mwalimu na watendaji wake wote,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!