Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zungu aukwaa uwaziri, Simbachawene amrithi Lugola
Habari za Siasa

Zungu aukwaa uwaziri, Simbachawene amrithi Lugola

Spread the love

RAIS John Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, kwa kumteua Mussa Zungu, Mbunge wa Ilala kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, akichukua nafasi ya George Simbachawene. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mabadiliko hayo yametangazwa leo tarehe 23 Januari 2020, na Katibu Mkuu  Kiongozi Ikulu, Balozi John Kijazi.

Kwa mujibu wa Balozi Kijazi, Simbachawene aliyemhamishia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, amechukua nafasi ya Kangi Lugola, ambaye uteuzi wake umetenguliwa leo na Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameteua mabalozi watatu, akiwemo Jenerali Jacob Kingu, aliyejiuzulu Ukatibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuwa Balozi.

Balozi Kijazi amesema  vituo vya kazi vya mabalozi hao, vitatangazwa baadae.

Pia, Balozi Kijazi amesema Rais Magufuli amewaongezea muda wa miaka 2, mabalozi saba, akiwemo Asha Rose Migiro, Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, George Madafa Balozi wa Tanzania nchini Italia na Emmanuel Nchimbi (Brazil).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!