Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Tanzania, Kenya zaungana kulinda rasilimali za mipakani
Kimataifa

Tanzania, Kenya zaungana kulinda rasilimali za mipakani

Spread the love

SERIKALI ya Kenya na Tanzania zimeungana kwa pamoja kulinda rasilimali za asili zilizoko katika mipaka ya nchi hizo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter jana tarehe 15 Januari 2019, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba ameandika kuwa, makubaliano hayo aliyasaini yeye pamoja na Waziri wa Mazingira na Misitu wa Kenya, Keriako Tobiko tarehe 29 Novemba 2018.

January ameandika kuwa, katika utekelezaji wa makubaliano hayo, wataangalia namna bora juu ya uhifadhi wa mazingira hasa katika maziwa ya Chala, Jipe, Natroni na Mto Mara.

Mambo mengine yatakayotekelezwa katika makubaliano hayo ni pamoja na uundwaji wa kamati ya pamoja kwa ngazi ya wizara ili kuratibu shughuli za usimamizi rasilimali za asili zilizoko mipakani, pamoja na kuanzisha timu ya wataalamu ili kutoa muongozo wa kiufundi katika usimamizi wa mipaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!