Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri wa Nishati ‘amtoa kafara’ mtumishi Tanesco
Habari Mchanganyiko

Waziri wa Nishati ‘amtoa kafara’ mtumishi Tanesco

Waziri wa Nishati na Madini, Merdad Karemani
Spread the love

WAZIRI wa Nishati na Madini, Merdad Karemani amemtoa  ‘kafara’ meneja uendeshaji wa mtambo wa kufua umeme wa Kidatu mkoani Morogoro kufuatia nchi kuingia gizani mara kwa mara kwa kukosa umeme kuanzia jana, anaandika Hamis Mguta.

Amefanya maamuzi ya kumtimua mtumishi kazi mtumishi huyo wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), leo alipofanya ziara katika gridi ya taifa eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam.

Karemani, katika ziara hiyo amemtaka Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Abdallah Ikwasa kumuondoa kazini mtumishi huyo kwa madai kwamba amekuwa mzembe.

 “Leo meneja wa Kidatu sitaki kumsikia akiwa kwenye kazi nataka kuona nani umemuweka, lakini aondoke kwanza, na wewe protection nimekupa siku tatu kuhakikisha unarekebisha mfumo wako, tunataka mtuambie nini kimetokea nini tuzuie ili kisitokee, hatuwezi kufanya kazi kwa mazoea, huwezi ondoka na nawaambia leo umeme ukizimika nataka kukuta barua nyie wenyewe mmeacha kazi” amesema.

Tazama Video hapo chini…..

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!