WAGOMBEA udiwani 169 kati ya 1145 ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioomba kuteuliwa kugombea udiwani kupitia chama hicho mkoani Kilimanjaro, wamepitishwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Moshi … (endelea).
Majina ya madiwani hao yametangaza rasmi jana tarehe 17 Agosti 2020 na Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya wakati akizungumza na vyombo vya habari mkoani humo baada ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.
”Wagombea hawa 169 ndio waliopendekezwa na kuteuliwa na kikao cha Halmashauri Kuu kwa ajili ya kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka huu,” amesema na kuongeza:
”Ni dhahiri kuwa, mchakato wetu wa kikatiba na kikanuni uliendelea baada ya kura za maoni kupigwa. Vikao vya uchujaji na utoaji mapendekezo viliendelea ambapo kamati zote za siasa kuanzia kata hadi mkoa zilikaa na kutoa maoni na mapendekezo yake.”
Leave a comment